Simba yapania kumaliza hasira kwa Namungo Fc

Joel JJ By Joel JJ β€’ 8th November 2023


Simba yapania kumaliza hasira kwa Namungo Fc

Kaimu Kocha Mkuu wa Simba Daniel Cadena amesema wachezaji wana ari na morali kubwa kuelekea mchezo wa ligi kuu dhidi ya Namungo Fc ambao utapigwa kesho Alhamisi katika uwanja wa Uhuru

Akizungumza katika Mkutano na Wanahabari mapema leo, Cadena alisema amezungumza na wachezaji wote, amewataka wasahau matokeo yaliyopita sasa ni wakati wa kuanza upya na kuwa bora zaidi

"Kabla sijaanza majukumu yangu, nilizungumza na wachezaji na kuwauliza kama wanataka niwe kocha wao au la? Kwa pamoja walisema wananihitaji kuwa kocha wao"

"Nikawaambia sasa tunapaswa kufanya kazi, tusahau matokeo ya mchezo uliopita, tuanze upya kwa kuboresha zaidi"

"Nafurahi kuona baada mazungumzo yetu kila mchezaji alikuwa tayari, wamefanya mazoezi kwa ari kubwa na wameonyesha wako tayari kwa mchezo dhidi ya Namungo ambao malengo yetu ni kupata ushindi," alisema Cadena

Akizungumza hali ya kiungo mshambuliaji Kibu Denis, Cadena amesema Kibu alipata majeraha kwenye mchezo dhidi ya Yanga lakini jana alianza mazoezi mepesi ya Gym

"Kibu ni mchezaji muhimu katika kikosi chetu, alipata majeraha kwenye mchezo uliopita, nimetaarifiwa na daktari wa timu kuwa anaendelea vizuri na jana alianza mazoezi ya Gym"

"Tutamuangalia baada ya mazoezi ya mwisho leo kuona yuko tayari au la. Lakini Simba ina wachezaji wengi ambao wote wana umuhimu. Hatutaangalia majina ya wachezaji, atakayepata nafasi ni yule ambaye anatuonyesha katika kiwanja cha mazoezi kuwa yuko tayari," alisema Cadena


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.