Tetesi za soka Ulaya, Jumapili Novemba 12 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 12th November 2023


Tetesi za soka Ulaya, Jumapili Novemba 12 2023

Kiungo wa kati wa Manchester City na Uingereza Kalvin Phillips, 27, anapendekeza kuhamia Newcastle kwa mkopo Januari badala ya klabu ya Juventus . (Calciomercato - in Italian)

Kiungo mshambuliaji wa Borussia Dortmund na Ujerumani Julian Brandt, 27, anawindwa na klabu za England Arsenal na Newcastle. (Mirror)

Chelsea wanapanga mazungumzo na Nottingham Forest ili kutatua mustakabali wa kiungo wa kati Mbrazil Andrey Santos, 19, ambaye yuko kwa mkopo katika kikosi cha Steve Cooper lakini amecheza mara moja pekee kwenye Premier League msimu huu. (Mirror)

Mshambulizi wa Ghana Andre Ayew, 33, amejiunga na Le Havre baada ya kuondoka Nottingham Forest mwishoni mwa msimu uliopita. (Fabrizio Romano)

Arsenal wamemfanya kiungo wa kati wa Aston Villa wa Brazil Douglas Luiz, 25, kuwa mshezaji nambari moja wanalenga kumnunua mwezi Januari. (Mirror)

Klabu ya Saudi Pro League Al-Ittihad iko kwenye mazungumzo ya juu na Mhispania mwenye umri wa miaka 57 na mkufunzi wa zamani wa Wolves na Real Madrid Julen Lopetegui. (Ben Jacobs

The Gunners walitaka kumtoa kiungo wa kati wa Ghana Thomas Partey, 30, lakini jeraha lake la paja lina maana kwamba anaweza kuendelea kubakia katika klabu hiyo baada ya kipindi cha majira ya baridi kali. (Football Insider)

Girona wanataka kumsajili tena kiungo wa kati wa Uhispania Oriol Romeu, 32 kutoka Barcelona . (90min)

Mkufunzi wa zamani wa Chelsea na Everton Frank Lampard yuko katika kinyang'anyiro cha kuwania nafasi ya ukocha katika klabu ya Oxford United ya League One . (Sun)

Manchester United wanavutiwa na mshambuliaji wa AZ Alkmaar raia wa Uholanzi Jayden Addi. (Football Transfers)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.