Manchester City wanavutiwa na mlinzi wa Chelsea na England Reece James, 23, kama mbadala wa muda mrefu wa mshirika mwenzake Kyle Walker, 33. (Independent, via Manchester Evening News)
Real Madrid bado wanamwania Beki wa Bayern Munich na Canada Alphonso Davies, 23. (Fabrizio Romano)
Liverpool na Tottenham watalazimika kulipa hadi £30m kumnunua mlinzi wa Bournemouth Muingereza Lloyd Kelly, 25, dirisha la uhamisho la Januari litakapofunguliwa. (Football Insider)
Inter Milan wanavutiwa na mshambuliaji wa Borussia Monchengladbach wa Uswizi Winsley Boteli, 17, ambaye pia ananyatiwa na Everton. (Inter Milan Live kupitia Liverpool Echo)
Liverpool wametuma maskauti wao huko Leeds mara kadhaa kumfuatilia kiungo wa Uingereza Archie Gray, 17. (Caught offside)
Winga wa Uhispania Nico Williams hataki kuondoka Athletic Bilbao na huenda akakubali kutia saini kandarasi mpya na klabu hiyo ya Uhispania, jambo ambalo litafanya iwe vigumu kwa Aston Villa kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 mwezi Januari. (Birmingham Live)
Barcelona wana nia ya kumsajili kiungo wa Nigeria Wilfred Ndidi, 26, mkataba wake na Leicester City utakapokamilika mwishoni mwa msimu huu. (Sky Sports)
Getafe wanataka mshambuliaji wa zamani wa Uingereza Mason Greenwood mwenye umri wa miaka 22 kusalia nao kwa mkopo kutoka Manchester United. (Sun)
Sir Jim Ratcliffe, ambaye anamiliki klabu ya Nice ya Ufaransa na anayetarajiwa kuwa mmiliki mpya wa Manchester United, ana nia ya kumleta kiungo wa kati wa Sweden Roony Bardghji mwenye umri wa miaka 17 kwenye klabu yake ya Ligue 1 baada ya kutoka kwenye benchi na kufunga bao la ushindi kwa FC Copenhagen dhidi ya United. Chelsea, Newcastle na Crystal Palace pia wanamwania. (Sun)
Ratcliffe, 71, anakaribia kufikia makubaliano ya £1.3bn kwa 25% ya hisa katika Manchester United. (Mail) Kiungo wa kati wa zamani wa Uhispania, Chelsea na Arsenal Cesc Fabregas, 36, anatazamiwa kuteuliwa kuwa kocha mkuu mpya wa Como katika nafasi yake ya kwanza ya ukocha mkuu. (Fabrizio Romano)
Chelsea wanatazamia kusajili mshambuliaji mwezi Januari licha ya kiungo wa kimataifa wa Senegal Nicolas Jackson, 22, kufunga mabao manne katika mechi zake mbili zilizopita za Ligi ya Premia. (Football Insider)
Mkufunzi wa Manchester City Pep Guardiola anasema "hatawahi" kumzuia mmoja wa wachezaji wake kuhamia kwa mpinzani, jambo ambalo linaweza kufungua njia kwa kiungo wa kati wa Uingereza Kalvin Phillips, 27, kujiunga na Liverpool au Newcastle. (Talksport)
Arsenal wanaweza kumtoa kiungo mshambulizi wa Uingereza Emile Smith Rowe, 23, katika mkataba utakaojumuisha pesa na mchezaji ili kumpata kiungo wa kati wa Aston Villa Mbrazil Douglas Luiz, 25. (football.london)
BBC



