Ahmed awapongeza mashabiki Simba, tuzo AFL

Joel JJ By Joel JJ β€’ 13th November 2023


Ahmed awapongeza mashabiki Simba, tuzo AFL

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally amesema mashabiki wa timu hiyo wanastahili pongezi kwa kushinda tuzo ya mashabiki bora wa michuano ya African Football League iliyofikia tamati jana huko Afrika Kusini

Ahmed amesema tuzo hiyo imetambua nguvu ya mashabiki wa Simba kwenye soka la Afrika ni wajibu wa kila Mwanasimba kulinda heshima hii waliyopewa na CAF kwa kuiunga mkono timu yao hata katika nyakati ngumu

"Hongereni sana wana Simba mnastahili heshima hii, mmeonesha tofauti ya mashabiki wa mpira na wanywa Supu za vibudu. Sifa hiii ya Ubora tunapaswa kuilinda na kujivunia maana sio kila mtu anaweza bora Kuilinda sifa hii ya ubora ni pamoja na kuwa wavumilivu pindi timu inapopitia nyakati ngumu"

"Tumewashinda mashabiki Wydad ambao huwa tunaamini bora, tumewashinda mashabiki wa Al Ahly ambao huwa tunaamini ni machizi soka, tumewashinda mashabiki wa Esparance ambao wanajua kushangilia kwelikweli. Tumewashinda Mashabiki wa Mamelod ambao pamoja na kuingia bure lakini hawafikii ubora wetu," alisema Ahmed

Tuzo hiyo ilipokelewa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi klabu ya Simba Salim Abdallah 'Try Again' katika hafla iliyofanyika jana baada ya mchezo kati ya Mamelodi Sundowns dhidi ya Wydad, mchezo uliowapa Sundowns ubingwa wa AFL


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.