Yanga yafuata kiungo mkabaji Ivory Coast

Joel JJ By Joel JJ β€’ 13th November 2023


Yanga yafuata kiungo mkabaji Ivory Coast

Klabu ya Yanga inatajwa kumuwania kiungo mkabaji tegemeo wa Racing Club ya Ivory Coast na timu ya taifa ya Ivory Coast ya vijana (U-20), Djire Abdoulaye

Djire mwenye umri wa miaka (18) amekuwa mchezaji tegemeo wa Racing Club licha ya umri wake kuwa mdogo

Kinda huyo pia anahusishwa na klabu za ASEC Mimosas na TP Mazembe

Yanga inasaka kiungo mkabaji ambaye atakuwa mbadala wa muda mrefu wa Khalid Aucho ambaye pamoja na ubora alionao, umri unamtupa mkono

Djire ni moja kati ya wachezaji waliounda Kikosi bora cha msimu cha ligi kuu ya Ivory Coast 21/22


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.