Simba yazindua chaneli ya WhatsApp

Joel JJ By Joel JJ β€’ 14th November 2023


Simba yazindua chaneli ya WhatsApp

Klabu ya Simba leo imetangaza kuzindua rasmi chaneli ya whatsApp ikiwa klabu ya kwanza kufikia hatua hiyo

Akizungumza katika mkutano na Wanahabari mapema leo, Mtendaji Mkuu wa Simba Imani Kajula alisema Simba ikiwa klabu yenye wafuasi zaidi kwenye mitandao kijamii kuliko klabu yoyote Tanzania, kupia WhatsApp Wanasimba watakuwa karibu zaidi ya timu yao kwa kupata taarifa muhimu kwa haraka

"Instagram tuna watu zaidi ya 5.5 milioni, Facebook zaidi ya 1.9 milioni, Twitter zaidi ya 1.5 milioni, YouTube tukiwa na zaidi ya 438k, kwenye app imepakuliwa zaidi ya laki saba na hivi karibuni tumeshinda tuzo ya mashabiki bora."

"Leo tunazindua Simba Sports Club WhatsApp channel. WhatsApp imepakuliwa na watu Bilioni 2.2 duniani ndio mtandao umepakuliwa zaidi duniani. WhatsApp wenyewe walitufata kuwa timu ya kwanza Afrika Mashariki na Kati kuwa na chaneli hii."

"Ni timu chache kama Kaizer Chiefs, Al Ahly, Barcelona, Real Madrid na Simba tumejiunga. Katika kuijaribu kabla ya kuzindua ndani ya wiki tumepata wafuasi laki moja. Faida kubwa ni mashabiki kupata taarifa na wadhamini wetu kuonyesha bidhaa zao."

"Hili ni lingine la kwanza kwa Simba kuwa karibu kwa Wenye Nchi. Simba inataka kuja kuwa timu namba moja Afrika na katika hili moja ya sehemu ya kuboresha ni namna ya kutoa habari."

"Tunapokuwa na chaneli kama hivi ni sehemu ya Wanasimba na watu wengine kupata taarifa sahihi za klabu. Hii ndio klabu ambayo inafanya vitu vyenye faida na tofauti."

"Ujio wa Simba WhatsApp Channel unakuja na ajira kwa mtu maalumu kuwa na kazi ya kutoa habari," alisema Kajula

Kajula pia aligusia mchakato wa kupatikana kocha mpya ambapo amesema mchakato huo uko kwenye hatua za mwisho

"Kuhusu kocha tupo kwenye mchakato wa mwisho"

SIMBA WHATSAPP CHANEL


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.