Newcastle United wanamtaka mshambuliaji wa Uhispania Ferran Torres, ambaye Barcelona wanajiandaa kumuuza baada ya mchezaji huyo wa zamani wa Manchester City, 23, kushindwa kufikia matarajio ya klabu hiyo ya La Liga. (Fichajes - Kwa Kihispania)
Chelsea, Liverpool na Manchester City wanamuwania beki wa Bayern Munich Alphonso Davies,23, lakini wanaamini mchezaji huyo anatamani sana kujunga Real Madrid. (90min)
Newcastle wanatafakari uwezekano wa kumnunua mlinzi wa Ujerumani na Bayer Leverkusen ambaye thamani yake inakadiriwa kuwa euro milioni Jonathan Tah, 27, Januari mwakani. (Sun)
Manchester United inakataa kumruhusu Jadon Sancho, 23, kuondoka kwa bei nafuu katika dirisha la uhamisho la Januari - licha ya meneja Erik ten Hag kutaka kumuondoa winga huyo wa Uingereza. (Mirror)
Chelsea wako tayari kushindana na Arsenal na Liverpool kwa ajili ya kumnunua kiungo wa kati wa Corinthians mwenye umri wa miaka 18 kutoka Amerika Kusini Gabriel Moscardo, ambaye anaweza £26m. (Standard)
Chelsea wako tayari kumenyana na Arsenal na Liverpool katika kinyang'anyiro cha kumnunua kiungo wa Corinthians mwenye umri wa miaka 18 kutoka Amerika Kusini Gabriel Moscardo, ambaye anaweza kugharimu takriban £26m. (Standard)
Mshambulizi wa Newcastle na England Callum Wilson, 31, atakuwa nje kwa karibu wiki sita kutokana na jeraha la misuli ya paja, huku mchezaji mwenzake wa Magpies, mlinzi wa Uholanzi Sven Botman, 23, akitarajiwa kuwa nje kwa muda mrefu zaidi kwa sababu ya tatizo la goti. (Telegraph - usajili unahitajika)
Manchester United wanaendelea kumfuatilia mshambuliaji wa Brighton Evan Ferguson, 19, licha ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Jamhuri ya Ireland hivi karibuni kusaini mkataba mpya na Seagulls. (Football Insider)
Mkurugenzi wa RB Leipzig Rouven Schroder amefungua mlango kwa mshambuliaji wa zamani wa Chelsea Timo Werner mwenye umri wa miaka 27 kuondoka katika klabu hiyo, huku Mjerumani huyo akiwa ameanza mechi mbili pekee msimu huu. (Standard)
Kuna mashaka kuhusu mustakabali wa mkurugenzi wa kandanda wa Manchester United John Murtough na mkurugenzi wa uendeshaji wa soka David Harrison kufuatia tangazo kwamba mtendaji mkuu Richard Arnold ataondoka katika klabu hiyo. (Mirror)
BBC