Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania Aisha Masaka ameweka historia ya kuwa Mtanzania wa kwanza kucheza ligi ya mabingwa Ulaya kwa upande wa wanawake
Masaka aliyewahi kutamba na Yanga Princess kabla ya kuuzwa huko Sweden, jana aliitumikia klabu yake ya Bk Hacken na kupata ushindi wa 2-1 wakiwa ugenini dhidi ya Paris FC ya nchini Ufaransa
Baada ya kuanza maisha yake kwa kusuasua huko Sweden, Masaka sasa ameimarika akijihakikishia muda zaidi wa kucheza kwenye kikosi cha kwanza
Katika msimu wa Ligi ya Wanawake ya Sweden iliyomalizika karibuni, Masaka alimaliza msimu akiwa na mabao matano

