Kikosi cha Simba kinaendelea na mazoezi Mo Simba Arena kujiandaa na mchezo wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Asec Mimosas utakaopigwa Jumamosi ijayo, Novemba 25 katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Ikiwa ni sehemu ya maandalizi, Simba inayonolewa na makocha wa muda Daniel Cadena na Seleman Matola, leo ilicheza mechi ya kirafiki dhidi ya Dar City
Simba iliibuka na ushindi wa mabao 4-0 katika mchezo huo uliopigwa Mo Simba Arena
Mabao ya Simba yalifungwa na Che Malone, Willy Onana, Israel Mwenda na Moses Phiri




