Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' kimerejea nchini kutoka Morocco ambako jana walifanikiwa kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Niger katika mchezo wa kuwania kufuzu kombe la Dunia 2026
Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh Gerson Msigwa aliwapokea Stars uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere na kuwakabidhi Tsh Milioni 10 zikiwa ni fedha za bonas ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa kila goli linalofungwa kwenye mechi za Kimataifa ambazo Stars au klabu zinashinda
Kuelekea mchezo dhidi ya Morocco utakaopigwa Jumanne, Msigwa amesema Rais Samia amenunua tiketi zote za Mzunguuko hivyo mashabiki wataingia bure katika mchezo huo utakaopigwa saa nne usiku



