Transfer - International

Tetesi za usajili Ulaya, Jumatatu Novemba 20 2023

Joel JJ By Joel JJ
20 Nov 2023
Tetesi za usajili Ulaya, Jumatatu Novemba 20 2023

Manchester United wako tayari kuongeza mara tatu mshahara wa Antoine Griezmann katika jitihada za kumsajili fowadi huyo wa Ufaransa, 32, kutoka Atletico Madrid mwezi Januari. (El Nacional, via Mundo Deportivo)

Juventus wanaweza kuwa tayari kumuuza winga Mwingereza Samuel Iling-Junior, 20, ambaye amekuwa akilengwa na Tottenham, katika dirisha la uhamisho la Januari. (Football Insider)

Aston Villa wanatafuta uwezekano wa kumnunua mshambuliaji wa Athletic Bilbao na Ghana Inaki Williams, 29 Januari. (Football Insider)

Mshambuliaji wa Ureno Bruno Fernandes, 29, amethibitisha kujitolea kwake kuendelea kuichezea Manchester United licha ya uvumi unaomhusisha na kuhamia Saudi Arabia. (90min)

Tottenham na Chelsea wana nia ya kumnunua Antonio Nusa anayelengwa na Fulham, 18, mshambuliaji wa Norway ambaye anawika sana katika klabu ya Club Brugge. (Football Insider)

Newcastle United inaweza kurejea tena kumnunua mshambuliaji wa Paris St-Germain Mfaransa Hugo Ekitike, 21, mwezi Januari. (Football Insider)

Barcelona watafanya uhamisho wa kumsajili kiungo wa kati wa Uhispania Martin Zubimendi, 24, ambaye anahusishwa na Arsenal, kutoka Real Sociedad msimu ujao. (Sport - in Spanish)

Roma wako tayari kufikiria ofa kwa beki wa kati wa zamani wa England Chris Smalling, 33, mwezi Januari. (Gazzetta dello Sport - in Italian)

AC Milan watajaribu kuimarisha safu yao ya ushambuliaji mwezi Januari na wanaweza kumnunua fowadi wa Lille na Canada Jonathan David, 23. (Gazzetta dello Sport - in Italian)

Barcelona na Real Madrid wanafikiria kumnunua winga wa Bayern Munich na Ujerumani Leroy Sane, 27. (Sport - in Spanish)

Real Madrid wanafikiria kumsajili mshambuliaji mwengine kwa mkopo au wa kudumu mwezi Januari baada ya Vinicius jnr, 23, kuumia akiwa na timu ya taifa ya Brazil, huku mshambuliaji wa RB Leipzig na Ujerumani Timo Werner, 27, akilengwa. (Sport - in Spanish)

Barcelona wanaweza kupokea hadi euro 5m (£4.4m) kama fidia baada ya kiungo Gavi, 19, kuumia akichezea Uhispania (Mundo Deportivo - in Spanish)

Wachezaji wa Ligi ya Premia wanaoitwa 'Big Six' wametakiwa kulipa zaidi 'kifurushi cha uokoaji' kwa piramidi ya soka ya Uingereza baada ya Everton kukatwa pointi 10. (Telegraph - subscription required)

BBC

More Stories

Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa uhuru
54m ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
57m ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
1h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
1h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
1h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
3h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
13h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
13h ago
READ MORE →
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
14h ago
READ MORE →
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
17h ago
READ MORE →