Transfer - International

Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi Novemba 23 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
23 Nov 2023
Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi Novemba 23 2023

Manchester United inajiandaa kuliuza kundi jingine la wachezaji 2024, huku zaidi ya wachezaji 10 wakitarajiwa kuondoka katika madirisha mawili ya uhamisho yajayo. (MEN) Kiasi cha wachezaji 15 wanaweza kuondoka United, huku winga wa Uingereza Jadon Sancho, 23, akitarajiwa kuwa wa kwanza kuondoka mwaka ujao. (Star)

Manchester City wanafanya kazi ya kumshawishi mshambuliaji Erling Haaland, 23, kusaini mkataba mpya, lakini makubaliano na mchezaji huyo wa kimataifa wa Norway hayajakaribia. (TeamTalk)

Newcastle United wanafuatilia hali ya Dominic Calvert-Lewin huko Everton huku mshambuliaji huyo wa Uingereza, 26, akiwa kwenye orodha ya wachezaji wanaotarajiwa kuwindwa msimu ujao. (TeamTalk)

Fulham wamewazidi Liverpool na Manchester United katika kinyang'anyiro cha kumnunua kiungo wa kati wa Fluminense wa Brazil Andre, 22, huku mshambuliaji wa Wolfsburg Mdenmark Jonas Wind, 24, pia akiwa miongoni mwa walengwa na klabu hiyo. (Standard)

Chelsea inawafuatilia mshambuliaji wa Feyenoord na Mexico Santiago Gimenez, 22, na winga wa Real Betis kutoka Senegal Assane Diao, 18, kwa kutarajia dirisha la uhamisho la Januari. (Football Transfers)

Arsenal wameamua kusajili mshambuliaji mpya mwaka 2024 - lakini biashara hiyo inaweza kusubiri hadi dirisha refu la majira ya kiangazi. (Football Insider)

Mazungumzo ya kiungo wa kati wa Italia Jorginho ya kuongeza mkataba na Arsenal yamekwama, kulingana na ajenti wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31. (mail)

Beki wa Club America na Uruguay Sebastian Caceres, 24, ameibuka kama usajili wa kipaumbele wa Tottenham katika dirisha la uhamisho la Januari. (football.London)

AC Milan wana nia ya kutaka kumnunua kwa mkopo beki wa Chelsea Benoit Badiashile mwenye umri wa miaka 22 wa Ufaransa, huku klabu hiyo ya Italia pia itawasiliana na Arsenal kuhusu kupatikana kwa mlinzi wa Poland Jakub Kiwior, 23. (Calciomercato - in Italian).

Chelsea wako tayari kumuuza mlinzi wa Uingereza Trevoh Chalobah, 24. (Football.London)

Manchester United inaweza kupigwa marufuku kutoka Uropa msimu ujao kutokana na ununuzi wa klabu hiyo na unaotarajiwa kufanywa na Sir Jim Ratcliffe, ambaye kundi lake la Ineos pia linamiliki klabu ya Nice ya Ufaransa. (Sun)

Kampuni ya uwekezaji ya Marekani ya 777 Partners inajiandaa kuingia tena kwenye mazungumzo na Everton kuhusu bei ya kuinunua baada ya klabu hiyo kupunguziwa pointi katika Ligi ya Premia. (Football Insider)

FA imethibitisha kuwa inachunguza madai ya ukiukaji mkubwa wa sheria za mawakala katika uhamisho unaohusisha Tottenham, Portsmouth na mshambuliaji wa zamani wa Uingereza Jermain Defoe. (Times – Subscription Required)

BBC

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
4h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
4h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
5h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
8h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
12h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
12h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
13h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
14h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
14h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
15h ago
READ MORE β†’