Tetesi za soka Ulaya, Jumamosi Novemba 25 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 25th November 2023


Tetesi za soka Ulaya, Jumamosi Novemba 25 2023

Newcastle wanapania kumsajili kwa mkopo kiungo wa Manchester City na Uingereza Kalvin Phillips mwenye umri wa miaka 27 na mshambuliaji wa Paris St-Germain Mfaransa Hugo Ekitike, 21, mwezi Januari. (Times- usajili unahitajika)

Brentford hawana mpango wa kumuuza mshambuliaji wa Uingereza Ivan Toney, 27, mwezi Januari licha ya Arsenal na Chelsea kumwania. (Mirror)

Manchester United wamemfanya mlinzi wa Everton wa England chini ya umri wa miaka 21 Jarrad Branthwaite, 21, kuwa shabaha yao kuu ya safu ya ulinzi mwaka 2024. (Teamtalk)

Klabu za ligi kuu ya Saudia zinafikiria kumnunua kiungo wa kati wa Manchester United na Denmark Christian Eriksen, 31, kwa pauni milioni 17 mwezi Januari. (Caught offside)

Leeds United wanajadiliana na kiungo wa Uingereza Archie Gray, na wanatazamiwa kupinga ombi la kumuuza mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 17 wakati wa uhamisho wa Januari huku Liverpool, Everton na Crystal Palace zikiwa miongoni mwa klabu wanazofikiriwa kumtaka. (Football Insider)

Real Madrid wanatazamiwa kumpa kocha Carlos Ancelotti, 64, kandarasi mpya ili kaw lengo la kusalia naye katika klabu hiyo huku Brazil ikionyesha nia ya kutaka kumsajili. (90 min)

Mkufunzi wa Barcelona Xavi amepinga tetesi kwamba kiungo wa kati wa Ujerumani Ilkay Gundogan, 33, ataondoka katika klabu hiyo kuelekea Saudi Arabia mwezi Januari. (Goal.com)

Bayern Munich wamewatangulia Manchester United na Chelsea katika mbio za kumwania mchezaji wa Schalke Mjerumani Assan Ouedraogo, 17. (Teamtalk)

AC Milan wanafikiria kumnunua beki wa Manchester City na Brazil Yan Couto, 21, ambaye yuko kwa mkopo katika klabu ya La Liga ya Girona. (Clciomercato)

Mshambuliaji wa Argentina Lautaro Martinez, 26, pia anatarajia kupewa ofa mpya na Inter Milan, baada ya kukataa kujiunga na Ligi ya Saudia msimu uliopita. (Tuttosport via Football Italia)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.