Kikosi cha Yanga kimerejea kutoka Algeria ambako juzi walicheza mechi ya kwanza ya hatua ya makundi dhidi ya CR Belouizdad na kupoteza kwa mabao 3-0
Wananchi wamerudi kujiandaa na mchezo unaofuata dhidi ya Al Ahly utakaopigwa Jumamosi, Disemba 02 katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Yanga inahitaji kushinda mchezo huo ili kuweka hai matumaini ya kufuzu robo fainali
Jana Al Ahly iliichapa Medeama bao 3-0 huko Misri sasa inaongoza kundi D ikiwa sawa na CR Belouizdad










