Mabosi Simba wateta na wachezaji

Joel JJ By Joel JJ β€’ 27th November 2023


Mabosi Simba wateta na wachezaji

Bodi ya Wakurugenzi ya klabu ya Simba ikiongozwa na Mwenyekiti Salim Abdallah 'Try Again' jana walifanya kikao na wachezaji

Kikao hicho kilihudhuhuriwa na viongozi wote waandamizi akiwemo Mwenyekiti wa klabu ya Simba, Murtaza Mangungu

Uongozi uliwapa nafasi wachezaji kuzungumza kila mmoja kueleza kama ipo changamoto inayowafanya wasifanya vizuri

Wachezaji wote walieleza kuwa hakuna changamoto yoyote ndani ya kambi na wameumizwa na mwenendo wa timu katika mechi zilizopita

Nyota wa Simba wamewaahidi Wanachama na Mashabiki kuwa watapambana kwa jasho na damu katika mechi zilizobaki kwenye ligi ya mabingwa ili kuhakikisha wanavuka hatua ya makundi

Wiki hii Simba itasafiri kwenda Botswana ambapo Jumamosi watachuana na Jwaneng Galaxy katika mchezo wa pili wa hatua ya makundi


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.