Bodi ya Wakurugenzi ya klabu ya Simba ikiongozwa na Mwenyekiti Salim Abdallah 'Try Again' jana walifanya kikao na wachezaji
Kikao hicho kilihudhuhuriwa na viongozi wote waandamizi akiwemo Mwenyekiti wa klabu ya Simba, Murtaza Mangungu
Uongozi uliwapa nafasi wachezaji kuzungumza kila mmoja kueleza kama ipo changamoto inayowafanya wasifanya vizuri
Wachezaji wote walieleza kuwa hakuna changamoto yoyote ndani ya kambi na wameumizwa na mwenendo wa timu katika mechi zilizopita
Nyota wa Simba wamewaahidi Wanachama na Mashabiki kuwa watapambana kwa jasho na damu katika mechi zilizobaki kwenye ligi ya mabingwa ili kuhakikisha wanavuka hatua ya makundi
Wiki hii Simba itasafiri kwenda Botswana ambapo Jumamosi watachuana na Jwaneng Galaxy katika mchezo wa pili wa hatua ya makundi













