Mambo ni magumu kwa Ihefu Fc

Joel JJ By Joel JJ β€’ 27th November 2023


Mambo ni magumu kwa Ihefu Fc

Ihefu Fc kutoka Mbarali mkoani Mbeya ina wakati mgumu baada ya kucheza mechi saba mfululizo pasipo ushindi katika ligi kuu ya NBC

Jana Ihefu Fc walilazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya JKT Tanzania ukiwa ni mchezo wao wa saba mfululizo bila ya ushindi

Mara ya mwisho Ihefu Fc kupata ushindi ilikuwa dhidi ya Yanga Oktoba 05 wakipata ushindi wa mabao 2-1 kwenye uwanja wao wa Highland Estates, Mbarali

Kocha Mkuu wa timu hiyo Moses Basena aliyechukua mikoba iliyoachwa na Zuberi Katwila aliyetimkia Mtibwa Sugar, bado hajaonja radha ya ushindi katika michezo mitano aliyoiongoza Ihefu

Katika mechi 7, Ihefu imeambulia sare mechi mbili tu na vipigo vitano. Inashika nafasi ya 13 kwenye msijmamo wa ligi ikiwa imekusanya alama 9


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.