Kocha Mkuu wa Simba Abdelhak Benchikha amekanyaga ardhi ya Tanzania usiku wa kuamkia leo na moja kwa moja kutambulishwa na uongozi wa Simba
Benchikha ametua nchini akiwa na Kocha Msaidizi Farid Zemiti na Kocha wa viungo Kamal Boudjenane
Watatu hao sasa wanakamilisha benchi la ufundi wakiungana na makocha wengine waliobaki
Daniel Cadena anarejea katika majukumu yake ya kocha wa magolikipa wakati Seleman Matola anarejea katika majukumu yake kwenye timu za vijana


