Transfer - International

Tetesi za soka Ulaya, Jumatano, Novemba 29 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
29 Nov 2023
Tetesi za soka Ulaya, Jumatano, Novemba 29 2023

Arsenal wako tayari kumwachia kipa wa England Aaron Ramsdale kuondoka mwishoni mwa msimu huu lakini hawatamruhusu mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 kuondoka wakati wa usajili la Januari. (90min)

Chelsea hawatakubali ombi la Fulham la kutaka kumnunua mshambuliaji wa Albania Armando Broja, 22, mwezi Januari. (Evening Standard)

Kiungo wa Uholanzi Donny van de Beek, 26, anasema ataondoka Manchester United Januari ikiwa hataanza kucheza mechi nyingi zaidi, akifichua kwamba uhamisho wa kuelekea Real Sociedad haukufaulu. (Diario AS, kupitia Sky Sports)

Manchester United wanatumai kuimarika katika nafasi nne mwezi Januari, ikiwa ni pamoja na safu ya ulinzi huku kukiwa na wasiwasi juu ya msimu wa kiungo wa Morocco Sofyan Amrabat mwenye umri wa miaka 27 hadi sasa. (Guardian)

Beki wa Ufaransa Raphael Varane, 30, na kiungo wa kati wa Uingereza Mason Mount, 24, ni miongoni mwa wachezaji wa Manchester United walio katika hatari ya kubadilishwa.Gurdian, via Express)

Bayern Munich wamejadili uwezekano wa kumsajili Varane kutoka Manchester United lakini hawaoni kama majadiliano hayo yatazaa matunda. (Sky Germany - kwa Kijerumani)

Tottenham wanavutiwa na kiungo wa kati wa Blackburn Rovers wa Uingereza Adam Wharton, 19. (90min)

Mshambuliaji wa Ukraine na Chelsea Mykhailo Mudryk, 22, anataka klabu hiyo kumsajili mchezaji mwenzake wa zamani wa Shakhtar Donetsk na timu ya taifa Georgiy Sudakov, 21, katika dirisha la uhamisho la Januari huku wawili hao wakionyesha ushirikiano mkubwa wakati walipokuwa pamoja Ukraine. (Gazzetta dello Sport - kwa Kiitaliano)

Mshambuliaji wa timu ya taifa ya England chini ya miaka 17, Mason Cotcher amekuwa akifanya mazoezi na kikosi cha kwanza cha Arsenal baada ya kuondoka Sunderland lakini The Gunners wanakabiliwa na ushindani kutoka kwa Rangers kuwania saini ya kinda huyo mwenye umri wa miaka 17. (Telegraph - usajili unahitajika)

Mshambuliaji wa Ujerumani Timo Werner, 27, yuko tayari kusalia RB Leipzig na kupigania nafasi yake kwenye kikosi badala ya kuhamia Manchester United Januari. (Metro)

Manchester United wanavutiwa na mlinda mlango wa Lazio Ivan Provedel, 29, lakini klabu hiyo ya Serie A itamuuza Muitaliano huyo kwa £30m pekee. (Il Messaggero, via Football Italia)

Chelsea hawajafikia makubaliano na Corinthians kumhusu Gabriel Moscardo mwenye umri wa miaka 18 na uhamisho wa Mbrazil huyo hauko karibu. (Fabrizio Romano)

Paris St-Germain na baadhi ya klabu zingine za Ligi ya Premia zinamtaka Moscardo huku Corinthians wakishikilia dau la £26m. (ESPN)

Winga wa Borussia Dortmund Donyell Malen, 24, bado analengwa na Liverpool huku meneja Jurgen Klopp akivutiwa sana na mchezaji huyo wa kimataifa wa Uholanzi. (Bild, via Teamtalk)

Arsenal wanafikiria kumnunua mshambuliaji wa Slovenia na RB Leipzig Benjamin Sesko, 20. (Football transferd)

Real Betis haijakata tamaa ya kumshawishi kiungo wa Argentina Guido Rodriguez, 29, kukataa Manchester United na Barcelona na kusalia na klabu hiyo ya Seville. (Marca kwa Kihispania)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’