Kocha Mkuu wa Miguel Gamondi amesema kikosi kimepata muda mzuri wa kufanya maandalizi ya mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Al Ahly ambao utapigwa kesho Jumamosi katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Akizungumza katika Mkutano na Wanahabari mapema leo, Gamondi alisema mchezo wa kwanza walikuwa na changamoto baadhi ya wachezaji kukabiliwa na uchovu kutokana na majukumu ya timu za Taifa lakini kuelekea mchezo wa kesho wamekuwa na muda mzuri wa kupumzika pamoja na kufanya maandalizi
"Nafurahi tumekuwa na muda mzuri wa kufanya maandalizi na kupata mapumziko hivyo kimsingi tuko tayari kwa mchezo dhidi ya Al Ahly"
"Tunajua utakuwa mchezo mgumu kwani tunakwenda kukabiliana na timu kubwa zaidi barani Afrika. Lakini nina imani na kundi hili la wachezaji nilionao wanaweza kushindana na Al Ahly katika ushindano uliosawa"
"Hapa Yanga tunasema Daima Mbele, Nyuma Mwiko, tunacheza 11 dhidi ya 11 hivyo nina imani tutakwenda kushindana na nina matumaini tutapata matokeo mazuri," alisema Gamondi
Aidha Gamondi aliongeza kuwa wamefanyia kazi makosa waliyofanya katika mchezo uliopita na jambo muhimu kwao kesho watahakikisha hawatarudia makosa hayo



