Fungia ya viwanja yakumba uwanja wa Ali Hassan Mwinyi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th December 2023


Fungia ya viwanja yakumba uwanja wa Ali Hassan Mwinyi

Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi uliopo mkoani Tabora umefungiwa kutumika kwa mchezo wowote wa Ligi Kuu mpaka pale utakaporekebishwa eneo la kuchezea, Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF) limeeleza

Taarifa iliyotolewa jana na shirikisho hilo imeeleza kuufungia uwanja huo mpaka pale utakapokaguliwa na kujiridhisha kufanyika kwa marekebisho hayo

TFF imesema uwanja huo umekosa vigezo vya kikanuni na sheria za soka hivyo kwa sasa hauwezi kutumika

Hatua hiyo itailazimu timu ya Tabora United kutafuta uwanja mwingine kwa michezo ya nyumbani hadi pale uwanja huo utakaporekebishwa

Aidha, TFF imezikumbusha timu zote kuendelea kutunza na kuboresha miundombinu ya viwanja kwa klabu ambazo hazimiliki viwanja


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.