Mchezo wa raundi ya tatu ligi ya mabingwa kati ya Wydad dhidi ya Simba uliopigwa uwanja wa Marrakesh umemalizika kwa Wydad kupata ushindi wa bao 1-0
Ni matokeo ya kuumiza sana kwani bao hilo wamefunga kwenye dakika za majeruhi
Kwa dakika zote 90 za mchezo Simba ilicheza vyema sana hata hivyo makosa yaliyofanyika dakika za majeruhi yameigharimu Simba kuacha alama zote tatu
Sio matokeo mazuri kwa Simba kwani ni wazi yanaongeza mlima katika malengo ya kufuzu hatua inayofuata
Bado alama tisa ziko mezani kushindaniwa zikiwemo mechi mbili uwanja wa nyumbani dhidi ya Wydad na Jwaneng
Mchezo unaofuata dhidi ya Wydad utapigwa Disemba 19, ni lazima kwa Simba kushinda mchezo huu






