Transfer - International

Tetesi za soka Ulaya, Jumatatu, Disemba 11 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
11 Dec 2023
Tetesi za soka Ulaya, Jumatatu, Disemba 11 2023

Raphael Varane huenda akaondoka Manchester United mwezi Januari kwa vile beki huyo wa zamani wa Ufaransa, 30, hana uhusiano mzuri na kocha Erik ten Hag. (Nicolo Schira)

Tottenham sasa wanaongoza Newcastle katika mbio za kumsajili winga Mwingereza Samuel Iling-Junior, 20, kutoka Juventus. (Football Insider)

Fulham wanaimarisha mpango wao wa kumnunua kiungo wa Le Havre raia wa Senegal Arouna Sangante, 21. (Sun

Fulham pia wameonyesha nia ya kutaka kumsajili kiungo wa Fluminense wa Brazil Andre, 22. (Nicolo Schira)

Liverpool ni miongoni mwa klabu za Ligi ya Premia zinazomtaka mshambuliaji wa Kijerumani Maximilian Beier, 21, ambaye anatarajiwa kuondoka Hoffenheim msimu ujao. (Sky Sports Ujerumani)

Everton wako tayari kumuuza beki wa England Ben Godfrey, 25, kwa Tottenham mwezi Januari iwapo dau litawasilishwa. (Football Insider)

Manchester United wametoa ofa ya kuongeza mara dufu mishahara ya beki wa Barcelona Ronald Araujo, 24, ambaye hana nia ya kuhamia Bayern Munich ,wezi Januari mwakani. (Mundo Deportivo - kwa Kihispania)

Mshambuliaji Mfaransa Mathys Tel, 18, ameamua kusalia Bayern Munich hadi msimu ujao, licha ya klabu kadhaa kutaka kumsajili kwa mkopo, ikiwa ni pamoja na Manchester United. (Sky Sports Germany)

Chelsea wamefanya mazungumzo na Palmeiras kuhusu dili la kumsajili winga wa Brazil Estevao Willian, 16, anayejulikana kama 'Messinho', ambaye pia amewavutia Barcelona. (Goal, via Mundo Deportivo - kwa Kihispania)

Mikel Arteta amemwalika gwiji wa Arsenal Dennis Bergkamp kurejea katika klabu kama sehemu ya wakufunzi wa chuo chao cha soka. (Football transfers)

BBC

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
1m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
30m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’