Klabu ya Singida Fountain Gates inadaiwa kuwa kwenye hatua za mwisho kukamilisha usajili wa mlinzi wa kushoto raia wa Botswana Benson Kitso Mangolo
Benson ambaye amewahi kuwa mchezaji bora wa mwaka nchini Botswana, anaitumikia Jwaneng Galaxy inayoshiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika
Mkataba wake na timu hiyo unafikia ukingoni Disemba 31 na atajiunga na Singida FG Januari 01 2024
Dirisha dogo la usajili litafunguliwa Disemba 16 na kufungwa Januari 15 hivyo ataweza kuitumikia Singida FG katika msimu huu
Hata hivyo kabla ya kukamilisha usajili wake Singida FG itapaswa kulipa madai ya wachezaji walioshinda kesi za madai dhidi ya timu hiyo FIFA
Beki Pascal Wawa ni miongoni mwa wachezaji wanaoidai Singida FG na haitaruhusiwa kusajili kama haitalipa madai yote



