Singida FG yanasa beki Botswana

Joel JJ By Joel JJ β€’ 12th December 2023


Singida FG yanasa beki Botswana

Klabu ya Singida Fountain Gates inadaiwa kuwa kwenye hatua za mwisho kukamilisha usajili wa mlinzi wa kushoto raia wa Botswana Benson Kitso Mangolo

Benson ambaye amewahi kuwa mchezaji bora wa mwaka nchini Botswana, anaitumikia Jwaneng Galaxy inayoshiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika

Mkataba wake na timu hiyo unafikia ukingoni Disemba 31 na atajiunga na Singida FG Januari 01 2024

Dirisha dogo la usajili litafunguliwa Disemba 16 na kufungwa Januari 15 hivyo ataweza kuitumikia Singida FG katika msimu huu

Hata hivyo kabla ya kukamilisha usajili wake Singida FG itapaswa kulipa madai ya wachezaji walioshinda kesi za madai dhidi ya timu hiyo FIFA

Beki Pascal Wawa ni miongoni mwa wachezaji wanaoidai Singida FG na haitaruhusiwa kusajili kama haitalipa madai yote


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.