Manchester United leo inakabiliwa na changamoto mbele ya Bayern Munich ili kukwepa kuondolewa kwenye Ligi ya Mabingwa barani Ulaya usiku wa leo
United itamenyana na Bayern Munich katika uwanja wa Old Trafford na inahitaji kumaliza rekodi ya klabu hiyo ya Ujerumani ya michezo 39 bila kushindwa katika hatua ya makundi ili kuwa na nafasi yoyote ya kutinga hatua ya mtoano
Lakini hata hiyo inaweza isitoshe, kwani timu ya Erik ten Hag iko mkiani mwa Kundi A na pia inahitaji sare kati ya Copenhagen na Galatasaray
"Ninachojua ni kwamba sifikirii kamwe hali mbaya. Tunafikiria chanya, tunajua la kufanya, lazima tushinde ili kubaki Ulaya, ni juu ya hilo, "Ten Hag alisema Jumatatu
"Tutaiandaa timu na hisia hiyo, kwa imani hiyo. Tumeonyesha katika wiki zilizopita tukiwa katika ubora wetu tunaweza kufanya hivyo"
Changamoto kubwa ya United msimu huu ni kutokuwa na muendelezo. Hilo lilionekana vyema wiki iliyopita wakati United ilipotoa mojawapo ya matokeo bora zaidi msimu huu kwa kuwalaza Chelsea 2-1 katikati ya wiki, lakini ikapoteza nyumbani kwa Bournemouth 3-0, na hivyo kusababisha dhihaka kubwa kutoka kwa mashabiki ndani ya Old Trafford
Kando na Ten Hag kwenye mkutano na wanahabari kabla ya mchezo wa mwisho wa kundi dhidi ya Bayern, kiungo wa kati Scott McTominay hakuweza kutoa maelezo kuhusu hali yao ya kutotabirika
Hata hivyo, alisisitiza kuwa wachezaji walikuwa nyuma ya meneja wao baada ya ripoti za hivi majuzi za machafuko katika vyumba vya kubadilishia nguo



