Mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu Ngao ya Jamii kwa Wanawake umemalizika kwa Yanga Princess kuibuka na ushindi dhidi ya Fountain Gate Princess kupitia changamoto ya mikwaju ya penati
Ni baada ya dakika 90 za mchezo huo kumalizika kwa suluhu ya bila kufungana na Yanga Princess kushinda mikwaju ya penati 4-2
Yanga Princess walipoteza mchezo wa nusu fainali dhidi ya Simba Queens kwa mikwaju ya penati 5-4 baada ya matokeo ya 0-0 wakati Fountain Gate Princess walichapwa mabao 5-0 na JKT Queens katika mchezo wa nusu fainali
Simba Queens na JKT Queens zinachuana katika mchezo wa fainali utakaopigwa saa 12 jioni