Transfer - International

Tetesi za usajili Ulaya, Jumatano Disemba 13 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
13 Dec 2023
Tetesi za usajili Ulaya, Jumatano Disemba 13 2023

Mazungumzo yatakayomwezesha kiungo wa Manchester United na timu ya taifa ya Uholanzi Donny van de Beek, 26, kujiunga na klabu ya Eintracht Frankfurt kwa mkopo yamepiga hatua. (Fabrizio Romano kwenye X)

Barcelona wanatazamia kumnunua kiungo wa Tottenham na timu ya taifa ya Argentina Giovani Lo Celso, 27 kwa mkopo dirisha la uhamisho litakapofunguliwa mweziJanuari . (90min).

Wamiliki wa Newcastle wanavutiwa na Jose Mourinho, huku kandarasi ya kocha huyo wa Roma mwenye umri wa miaka 60 ikitarajiwa kumalizika msimu ujao baada ya tetesi kuibuka kuwa klabu hiyo ya Serie A haina nia ya kusalia naye kama mkufunzi wao. (Gazzetta dello Sport - kwa Kiitaliano)

Getafe wanatumai kumnunua mshambuliaji wa Uingereza Mason Greenwood, 22, kutoka Manchester United na watafaidika kutokana na kipengele cha mauzo cha 20% ambacho kiliwekwa katika mkataba wake wa mkopo kwa klabu hiyo ya La Liga. (Athletic-Usajili unahitajika)

Arsenal wametoa ofa ya pauni milioni 17.2 pamoja na nyongeza kwa mshambuliaji wa Santos na Brazil wa chini ya umri wa miaka 20 Marcos Leonardo, 20. (Fichajes - kwa Kihispania).

Manchester City wanaweza kumnunua kiungo na mshambuliaji dirisha la uhamisho a wachezaji litakapofunguliwa mwezi Januari. (Football Insider)

Juventus bado wana nia ya kumsajili kiungo wa Manchester City na Uingereza Kalvin Phillips, 28, kwa mkopo mwezi Januari. (Gazzetta dello Sport - kwa Kiitaliano)

Chelsea wanamtaka mshambuliaji wa Sporting Lisbon na Uswidi Viktor Gyokeres, 25. (Ekrem Konur on X)

Kocha wa zamani wa Wolves na Uhispania Julen Lopetegui, 57, anawaniwa na klabu za Crystal Palace na Nottingham Forest. Mhispania huyo hajafanikiwa kupata kazi tangu aondoke Wolves mwezi Agosti. (Sun)

Beki wa Liverpool Mfaransa Ibrahima Konate, 24, ameanza mazungumzo ya kuongeza mkataba na The Reds, licha ya uvumi unaomhusisha na kuhamia Paris St-Germain. (le10sport - kwa Kifaransa)

Wasaka vipaji wa Ligi ya Premia kutoka Manchester United, Manchester City, Tottenham na Liverpool wanamfuatilia kiungo wa kati wa Middlesbrough Hayden Hackney, 21, kwa matarajio kwamba ataondoka katika klabu hiyo msimu ujao. (Mail)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
45m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’