Aliyekuwa Kocha Mkuu wa Namungo Fc, Denis Kitambi ameachana rasmi na klabu hiyo
Taarifa za Kitambi kuachana na Namungo zilianza kuvuma jana kwenye mitandao ya kijamii na hatimaye leo Namungo Fc wamethibitisha kupitia taarifa waliyoitoa kwa Umma
"Uongozi wa Namungo Fc unapenda kumshukuru Kocha Denis Kitambi kwa muda wote aliotumikia timu kwa ushirikiano mkubwa ndani ya Timu yetu"
"Namungo Fc inamtakia kila la kheri Kocha Denis Kitambi katika safari yake ya ukocha nje ya Namungo Fc," ilisema taarifa ya Namungo Fc
Kitambi ambaye alijiunga na Namungo Fc msimu uliopita, mwanzoni mwa msimu huu alibadilishiwa majukumu na kuwa kocha msaidizi baada ya Namungo kumuajiri Cedric Kaze kuwa kocha mkuu
Hata hivyo Kaze alibwaga manyanga baada ya kukosa ushindi katika mechi tano za mwanzo msimu huu na majukumu ya ukocha kurejeshwa kwa Kitambi