Yanga yamtambulisha Shekhan

Joel JJ By Joel JJ β€’ 16th December 2023


Yanga yamtambulisha Shekhan

Yanga imemtambulisha rasmi kiungo mshambuliaji Shekhan Ibrahim Khamis aliyesajiliwa kutoka klabu ya JKU

Kwa takribani siku nne usajili wa Shekhan ulitawala mitandao ya kijamii kutokana na vile usajili huo ulivyokamilishwa na Makamu wa Rais wa Yanga Arafat Haji

Shekhan ametua Yanga kwa mkataba wa miaka mitatu na anakuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na Yanga katika dirisha dogo la usajili

Nyota huyo anatarajiwa kutambulishwa kwa mashabiki wa Yanga kabla ya mchezo wa Ligi Kuu ambao Yanga watacheza na Mtibwa Sugar baadae leo katika uwanja wa Azam Complex


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.