Kombe la Dunia la klabu 2025 kushirikisha timu 32

Joel JJ By Joel JJ β€’ 18th December 2023


Kombe la Dunia la klabu 2025 kushirikisha timu 32

Mwaka 2025 michuano ya kombe la Dunia kwa klabu itafanyika nchini Marekani ambapo Afrika imepewa nafasi ya kupeleka timu nne katika michuano hiyo itakayoshirikisha timu 32

Afrika imepewa nafasi nne ambapo nafasi mbili tayari zimechukuliwa na Al Ahly na Wydad zilizoshinda taji la Ligi ya Mabingwa barani Afrika katika miaka minne iliyopita

Timu mbili (ukitoa Al Ahly na Wydad) ambazo zitakusanya alama nyingi katika ranking za CAF baada ya michuano ya ligi ya mabingwa ya mwaka huu basi zitaungana na Al Ahly na Wydad kushiriki michuano hiyo

Lakini pia timu itakayotwaa taji la Ligi ya Mabingwa msimu huu (kama sio Al Ahly, Wydad) itakuwa imekata tiketi moja kwa moja ya kushiriki michuano hiyo

Klabu za Simba na Yanga zinaweza kukata tiketi ya kushiriki michuno hiyo kama zitafanikiwa kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa msimu


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.