Mwaka 2025 michuano ya kombe la Dunia kwa klabu itafanyika nchini Marekani ambapo Afrika imepewa nafasi ya kupeleka timu nne katika michuano hiyo itakayoshirikisha timu 32
Afrika imepewa nafasi nne ambapo nafasi mbili tayari zimechukuliwa na Al Ahly na Wydad zilizoshinda taji la Ligi ya Mabingwa barani Afrika katika miaka minne iliyopita
Timu mbili (ukitoa Al Ahly na Wydad) ambazo zitakusanya alama nyingi katika ranking za CAF baada ya michuano ya ligi ya mabingwa ya mwaka huu basi zitaungana na Al Ahly na Wydad kushiriki michuano hiyo
Lakini pia timu itakayotwaa taji la Ligi ya Mabingwa msimu huu (kama sio Al Ahly, Wydad) itakuwa imekata tiketi moja kwa moja ya kushiriki michuano hiyo
Klabu za Simba na Yanga zinaweza kukata tiketi ya kushiriki michuno hiyo kama zitafanikiwa kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa msimu



