Yanga yamrejesha Okrah Magic Tanzania

Joel JJ By Joel JJ β€’ 29th December 2023


Yanga yamrejesha Okrah Magic Tanzania

Taarifa kutoka nchini Ghana zimebainisha kuwa winga wa Bechem United Augustine Okrah tayari amemalizana na Yanga

Wakati Wananchi wakisubiri utambulisho wa mchezaji mpya visiwani Zanzibar, imeelezwa kuwa Okrah tayari yuko Zanzibar

Okrah ndiye kinara wa mabao Ligi kuu ya Ghana akipachika mabao tisa kwenye mechi 16 alizocheza msimu huu

Okrah amewahi kuitumikia Simba msimu uliopita akifunga mabao manner katika ligi kuu ya NBC

Anaweza kutumika katika michuano ya ligi ya mabingwa hivyo kama atasajiliwa na Yanga anaweza kuongezwa iwapo Wananchi watatinga robo fainali


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.