Klabu ya Namungo imemtambulisha Mwinyi Zahera kuwa kocha mkuu wa timu hiyo. Namungo kutokea mkoani Lindi ilikuwa inanolewa na kocha Denis Kitambi ambaye ametimkia Geita Gold FC
Mwanzoni mwa msimu Zahera aliinoa Coastal Union kabla ya timu hiyo kuachana nae baada ya mechi sita bila ushindi
Zahera kocha wa zamani wa Yanga, pia amewahi kuinoa klabu ya Polisi Tanzania ambayo ilishuka daraja msimu uliopita



