Kocha wa Liverpool Jurgen Klopp amesema hamuombei mema mchezaji wake Mohamed Salah kuelekea mashindano ya Mataifa ya Afrika βAFCONβ yanayotarajiwa kuanza Ivory Coast Januari 13
Salah atakuwa nje ya kikosi cha Liverpool kwa ajili ya kulitumikia taifa lake la Misri kwenye AFCON
Vilevile Wataru Endo ambaye ni kapteni wa Timu ya Taifa ya Japan atakuwa kwenye majukumu ya timu hiyo kwenye mashindano ya Asian Cup yatakayofanyika Qatar kuanzia Januari 12
Ikiwa mataifa ya wachezaji hawa yatafanya vizuri kwenye mashindano haya, Liverpool italazimika kusubiri hadi wiki ya pili ya Februari mwaka huu ili kupata huduma zao
Hii ndio sababu Klopp kufichua kwamba hawatakii mema na anaombea watolewe mapema ili zaidi ni kuona wanarudi wakiwa wazima tu.