Mchezaji wa kiungo cha kati wa England Jordan Henderson, mwenye umri wa miaka 33, anataka kurudi katika ligi kuu ya England kutoka timu ya Saudi Arabia Al Ettifaq na atazingatia kwa uzito mapendekezo yoyote yatakayowasilishwa kwa klabu hiyo mwezi huu. (Mail)
Conor Gallagher anatarajiwa kusalia Chelsea mwezi huu licha ya Tottenham kutaka kumsajili mchezaji huyo wa kiungo cha kati wa timu ya England mwenye umri wa miaka 23. (Mirror)
Huenda Chelsea ikawasilisha pendekezo kwa ajili ya Henderson, jambo ambalo linaongeza uwezekano wa Galagher kuondoka. (football.london)
Manchester United inataka kumsajili mchezaji wa kiungo cha kati wa Crystal Palace Michael Olise, mwenye umri wa miaka 22, na huenda ikatumia mlinzi wa England Aaron Wan-Bissaka, mwenye umri wa miaka 26, kama sehemu ya makubaliano hayo. (Star)
Wolves inaangalia uhamisho wa mkopo katika dirisha la uhamisho mwezi Januari wakati Danny Ings mwenye umri wa miaka 31 wa West Ham akiwa miongoni mwa walengwa wakuu. (Telegraph)
Everton inajaribu kuipiku Sevilla katika kumwania kwa mkopo mchezaji wa kiungo cha kati wa Tunisia mwenye umri wa miaka 20 Hannibal Mejbri kutoka Manchester United. (Fabrizio Romano)
West Ham inafikiria kumwania winga wa Ajax na timu ya taifa ya Uholanzi Steven Bergwijn, mwenye umri wa miaka 26. (Sun)
Manchester City wapo tayari kusubiri mpaka majira ya joto kabla ya kujaribu kumsajili mchezaji wa Bayern Munich na timu ya taifa ya Ujerumani Joshua Kimmich mwenye umri wa miaka 28 katika ombi la kutaka kumsajili kwa gharama iliopungua. (Mirror)
Kevin de Bruyne wa Manchester City na timu ya taifa ya Ubeligiji anaendelea kusakwa sana na klabu kuu za ligi ya Saudia katika dirisha la uhamisho kwenye majira ya joto. (Football Insider)
Juventus inajaribu kufikia makubaliano ya kibinfasi na beki wa kati wa timu ya Lille raia wa Ureno Tiago Djalo, mwenye umri wamiaka 23 ambaye pia anasakwa na Inter Milan. (Fabrizio Romano)
Bayern Munich haijakata tamaa kumwania mlinzi wa Barcelona na timu ya taifa ya Uruguay Ronald Araujo licha ya kwamba ombi la mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 huenda lisikubaliwe katika dirisha la uhamisho la Januari. (Sky Sports Germany)
Meneja wa Arsenal Mikel Arteta huenda asimrudishe mlinzi wa Uskotchi Kieran Tierney, mwenye umri wa miaka 26, kutoka kwa uhamisho wa mkopo na Real Sociedad katika dirisha la uhamisho Januari. (Football Insider)
BBC



