Baada ya TFF kutoa orodha ya mwisho ya wachezaji 27 ambao wanakwenda kushiriki michuano ya Afcon 2023 itayoanza wiki ijayo nchini Misri, Yanga iimetoa jumla ya wachezaji saba katika Mataifa mbalimbali wanaokwenda kushiriki michuano hiyo
Katika timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars', Ibrahim Bacca, Dickson Job, Bakari Mwamnyeto na Mudathir Yahya wamepenya katika orodha ya mwisho
Djigui Diarra (Mali), Stephane Aziz Ki (Burkina Faso) na Kennedy Musonda Zambia wanakamilisha idadi ya wachezaji 7 wa Yanga ambao watakuwa Ivory Coast
Yanga ni miongoni mwa timu zilizotoa wachezaji wengi katika michuano hiyo
Mamelodi Sundowns wanaongoza wakitoa wachezaji 11, Al Ahly ikitoa wachezaji 10, Pyramids wachezaji 9 na Yanga ikitoa wachezaji 7
Klabu ya Simba imetoa wachezaji ambapo wanne katika timu ya Taifa ya Tanzania na wawili wa nje
Aishi Manula, Mohammed Hussein, Mzamiru Yassin na Kibu Denis wamepenya katika orodha ya mwisho ya Stars wakati Clatous Chama akijumuishwa Zambia na Hennock Inonga (DR Congo)