Ajax wana nia ya kumsajili kiungo wa kati wa Uingereza Jordan Henderson kutoka klabu ya Saudi Pro League Al-Ettifaq lakini wanakabiliwa na ushindani kutoka kwa vilabu vya Premier League na Bundesliga kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 . (ESPN)
Al-Ettifaq haitashinikizwa kumuuza Henderson mwezi Januari, au kumruhusu kuondoka kwa mkopo, huku nahodha huyo wa zamani wa Liverpool akiwa na mazungumzo na meneja Steven Gerrard na mkurugenzi wa michezo Mark Allen (Talksport)
Winga wa Uingereza Jadon Sancho, 23, anatazamiwa kujiunga na Borussia Dortmund kwa mkopo lakini atarejea katika klabu yake ya Manchester United baada ya kuitumikia kwa sababu klabu hiyo ya Ujerumani haiwezi kumudu kufanya mkataba huo kuwa wa kudumu.(Mirror)
Bayern Munich wamewasilisha ombi la kuchelewa kumnunua mchezaji anayelengwa na Tottenham Radu Dragusin na sasa utakuwa uamuzi wa beki huyo wa Genoa na Romania mwenye umri wa miaka 21 kuamua ni wapi anataka kuhamia (Sky Sports)
Rais wa Paris St-Germain Nasser Al-Khelaifi anasema anataka mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe mwenye umri wa miaka 25, ambaye kandarasi yake inamalizika msimu wa joto, kusalia na mabingwa hao wa Ufaransa kwa kuwa ndio klabu bora kwake. (RMC Sport - kwa Kifaransa)
PSG wanashughulikia mpango wa kumsajili kiungo wa kati wa Ujerumani Joshua Kimmich mwenye umri wa miaka 28 kutoka Bayern Munich mwezi Januari. (Sky Germany - kwa Kijerumani)
Newcastle United itakataa ofa zozote za Januari kutoka kwa PSG kwa kiungo wa kati wa Brazil Bruno Guimaraes huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 akitua Tyneside. (The i)
Mshambulizi wa kimataifa wa Uingereza Cole Palmer, 21, anasema alitaka kuhama kwa mkopo kutoka Manchester City msimu uliopita lakini akaambiwa anaweza "kusalia au uuzwe" kabla ya kujiunga na Chelsea. (Sky Sports)
Fulham inamfuatilia mshambuliaji wa AZ Alkmaar na Ugiriki Vangelis Pavlidis , 25 , ambaye amekuwa akitazamwa na Chelsea, AC Milan na Barcelona wiki za hivi karibuni. (Evening Standard)
Mkufunzi wa Leicester City Enzo Maresca anashinikiza kumnunua kiungo wa kati wa Italia Stefano Sensi mwenye umri wa miaka 28 kutoka Inter Milan. (Sky Sports Italia - kwa Kiitaliano)
Barcelona wamesitisha mazungumzo kuhusu mustakabali wa mshambuliaji wa Atletico Madrid anayecheza kwa mkopo Joao Felix, huku klabu hiyo ya Uhispania ikiwa na mashaka kuhusu mchezaji huyo wa kimataifa wa Ureno mwenye umri wa miaka 24 kwa sababu ya kushuka kiwango chake. cha mchezo(Sport - kwa Kihispania)
Juventus wanapanga kukutana na winga Mwingereza Samuel Iling-Junior kujadili kuhusu kuongezwa kwa kandarasi ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20, ambaye mkataba wake wa sasa unakamilika 2025. (Tuttosport - in Italian)
Tottenham wako tayari kujiunga na kinyang'anyiro cha kumnunua kiungo wa Middlesbrough Hayden Hackney na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 pia akizivutia Manchester City, Manchester United na Liverpool. (Evening Standard)
BBC



