Mjadala mkubwa ulioibuka katika mitandao ya kijamii ni matukio ya yaliyojiri kwenye kombe la Mapinduzi kwa waamuzi kushindwa kutafsiri vyema sheria 17 za soka na hivyo kuzinufaisha timu ambazo hazikustahili
Pengine katika michuano ya mwaka huu ndio imeshuhudia makosa mengi yakifanywa na waamuzi kuliko wakati mwingine wowote tangu michuano hiyo ilipoanzishwa
Jana Kamati ya waamuzi ya michuano hiyo ilitangaza kumfungia mwamuzi wa kwanza msaidizi Yusuf Shombe Issa kwa kushindwa kutafsiri vizuri sheria kwa kuruhusu bao la kwanza la Azam na baadaye Singida Fountain Gate ambayo hayakuwa halali katika mchezo wa robo fainali
Azam iliandika bao la kwanza kupitia kwa Alassane Diao kwa kichwa akionekana ameotea kabla ya Singida kupata bao la pili lililofungwa na Habib Kyombo akionekana pia ameotea na kufanya matokeo ya mwisho Singida kushinda 2-1 na kutinga nusu fainali
Mbali na Issa, pia Shekha alisema mwamuzi wa pili aliyefungiwa ni Mohamed Mwadini aliyekuwa mwamuzi wa kwanza msaidizi ambaye aliruhusu bao katika mchezo wa makundi kati ya JKU na APR akidai mpira ulivuka mstari wa goli wakati haikuwa hivyo
Mechi hiyo iliisha kwa APR kushinda mabao 3-1 na kwenda robo fainali ambako ilifanikiwa kuiondosha Yanga kabla ya kutolewa na Mlandege katika nusu fainali
Katika mchezo wa nusu fainali kati ya Singida FG dhidi ya Simba madudu mengine yakafanyika Singida FG wakipoteza mchezo huo kupitia mikwaju ya penati
Licha ya kuongezwa dakika 6 baada ya dakika 90 kumalizika, mchezo ulichezwa kwa takribani dakika 100 Simba ikisawazisha bao katika dakika ya 9 kati ya 10 zilizochezwa kupitia mpira wa kona ambao ulikuwa na utata
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Waziri Shekha amesema baada ya kikao kilichofanyika leo Januari 11, 2024 kupitia ufanisi uliofanywa mwamuzi Msomali na wasaidizi wake wamegundua kwamba mwamuzi huyo hakuwa sahihi kwenye uamuzi wake huo wa kuwapa kona Simba ambayo ilizaa bao la kusawazisha
Shekha amesema kosa hilo ni la kibinadamu kwani waamuzi nao hufanya makosa



