Hatimaye michuano ya kombe la Mapinduzi iliyoanza kutimua vumbi Disemba 28 2023, inahitimishwa leo kwa mchezo wa fainali kupigwa kati ya Mlandege dhidi ya Simba
Ni saa 2:15 usiku mchezo wa fainali utapigwa katika uwanja wa New Amaan Complex bingwa wa michuano hiyo akiondoka na kitita cha Tsh Milioni 100
Simba itakuwa ikiwania taji la tano la michuano hiyo wakati Mlandege Fc ambao ndio mabingwa watetezi, wanawania taji la pili
Pamoja na Simba kupewa nafasi ya kutwaa ubingwa kutokana na ubora wa kikosi chake, lakini hakuna mechi rahisi ya fainali
Kocha Mkuu wa Simba Abdelhak Benchikha atakuwa akiwania taji lake la kwanza tangu alipojiunga na Simba
Baada ya kutwaa Ngao ya Jamii mwanzoni mwa msimu, hii ni nafasi nyingine kwa Simba kuongeza taji la pili kabatini katika msimu huu
Mlandege watakuwa na faida ya kucheza katika ardhi ya nyumbani na pengine watakuwa na sapoti ya kutosha licha ya ukubwa wa Simba