Manchester United wanatakiwa kulipa pauni milioni 52 ili kumnasa beki wa kati wa klabu ya Nice na timu ya Taifa ya Ufaransa Jean-Clair Todibo, 24, ambaye wanavutiwa na kiwango chake.(Caught Offside)
United pamoja na Chelsea wanavutiwa na mshambuliaji kinda wa Sweden Jonah Kusi-Asare mwenye miaka 16 anayecheza katika klabu AIK.
Bayern Munich pia wanavutiwa na kinda huyo. (HITC) United pia wameanza mipango ya awali kumnasa kiungo kinda wa Ubelgiji Arthur Vermeeren, 18, kutoka klabu ya Royal Antwerp. (Football Insider)
Newcastle wapo tayari kumuachia mwishoni mwa msimu kiungo wao kutoka Brazil Bruno Guimaraes, 26, join kujiunga na Barcelona ama Real Madrid kwa dau la chini ya pauni milioni 100. (Football Transfers)
Juventus wamefanya mazungumzo na kiungo wa England Jordan Henderson, 33, juu ya uwezekano wa kumsajili kwa mkopo kutoka klabu ya Al-Ettifaq ya Saudia. (Gianluca Di Marzio - in Italian)
Klabu ya Ajax ya Uholanzi nayo inasukuma kete zake kujaribu kumnasa Henderson ambaye anatarajiwa kufanya mazungumzo ya mustakabali wake na uongozi wa klabu yake. (Standard)
Klabu ya Tottenham inapanga kumrejesha kiungo wake Tanguy Ndombele, 27, kutoka klabu Galatasaray anapocheza kwa mkopo kwa sababu ya kutokuwa na uhakika wa kumnasa Conor Gallagher kutoka Chelsea. (Football Transfers)
Italazimika Wolves kupewa “kitita cha kurusha cha pesa” ili kumuuza kiungo wao raia wa Brazil Joao Gomes, 22, katika dirisha la usajili la mwezi Januari. Tottenham wanaripoti wa kuvutiwa na mchezaji huyo. (Mirror)
Klabu ya Napoli imetuma dau la usajili kwa kiungo wa klabu ya Bournemouth na timu ya taifa ya Ivory Coast Hamed Traore, 23. (Fabrizio Romano)
Sweden wamefanya mazungumzo na kocha wa zamani wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer juu ya uwezekano wa kuinoa timu ya taifa hilo la Scandinavia. (Fotboll Skanalen - in Swedish)
BBC



