Mlandege mabingwa kombe la Mapinduzi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 13th January 2024


Mlandege mabingwa kombe la Mapinduzi

Mlandege wametetea kombe la Mapinduzi kwa msimu wa pili mfululizo baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Simba katika mchezo wa fainali uliopigwa uwanja wa New Amaan Complex

Bao pekee la Mlandege lilifungwa na Joseph Akandwanao raia wa Jamaica kwenye dakika ya 54

Ulikuwa mchezo wa upande mmoja kwa muda mwingi Simba ikitawala lakini bado changamoto ya Simba ni ileile, kushindwa kutumia nafasi

Simba inaondoka Zanzibar na kitita cha Tsh Milioni 70 baada ya kumaliza nafasi ya pili huku Mlandege wakibeba Tsh Milioni 100 za ubingwa


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.