Mlandege wametetea kombe la Mapinduzi kwa msimu wa pili mfululizo baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Simba katika mchezo wa fainali uliopigwa uwanja wa New Amaan Complex
Bao pekee la Mlandege lilifungwa na Joseph Akandwanao raia wa Jamaica kwenye dakika ya 54
Ulikuwa mchezo wa upande mmoja kwa muda mwingi Simba ikitawala lakini bado changamoto ya Simba ni ileile, kushindwa kutumia nafasi
Simba inaondoka Zanzibar na kitita cha Tsh Milioni 70 baada ya kumaliza nafasi ya pili huku Mlandege wakibeba Tsh Milioni 100 za ubingwa



