Wenyeji Ivory Coast wameanza vyema michuano ya Afcon 2023 kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Guinea-Bissau mjini Abidjan
Seko Fofana na Jean-Philippe Krasso walitumia nafasi kuifungia timu yao mabao hayo muhimu
Ivory Coast haikuwa bora sana katika mchezo huo lakini jambo muhimu kwao ni ushindi mbele ya mashabiki wao
Mechi tatu zitapigwa leo, Nigeria watachuana na Guinea ya Ikweta saa 11 jioni, Misri dhidi ya Msumbiji saa 2 usiku na mchezo wa tatu ni kati ya Ghana dhidi ya Cape Verde saa 5 usiku