Tanzania - Taifa Stars - Yanga - Simba - Azam - Local

Afcon : 2023; Tanzania kuanza na Morocco Jumatano

Joel JJ By Joel JJ
β€’
15 Jan 2024
Afcon : 2023; Tanzania kuanza na Morocco Jumatano

Michuano ya Afcon 2023 tayari imeanza Ivory Coast mpaka sasa baadhi ya mechi zikitoa matokeo yasiyotarajiwa na wengi

Katika mechi nne zilizochezwa mpaka sasa, mechi mbili zimetoa washindi huku mechi mbili zikimalizika kwa sare

Wenyeji Ivory Coast walianza vyema michuano hiyo kwa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Guinea Bissau

Mechi nyingine tatu zikapigwa jana, Guinea ya Ikweta ikapata sare ya bao 1-1 dhidi ya Nigeria katika mechi ambayo wengi waliamini Nigeria ingeshinda

Misri ikaponea chupuchupu mbele ya Msumbiji ikilazimishwa sare ya mabao 2-2 huku Ghana wakiangukia pua mbele ya Cape Verde wakichapwa mabao 2-1

Leo mechi nyingine tatu zitapigwa ambapo Senegal watachuana na Gambia saa 11 jioni, Cameroon watachuana na Guinea saa 2 usiku na Algera wakichuana na Angola saa 5 usiku

Tanzania itatupa karata yake ya kwanza siku ya Jumatano kwa mchezo dhidi ya Morocco mchezo utakaopigwa saa 2 usiku

Kwa matokeo ya mechi hizi za mwanzo, unaweza kusema hakuna lisilowezekana, Tanzania nayo ina nafasi ya kupata matokeo dhidi ya Morocco

Kama wachezaji wa Stars watajitoa na kujituma kwa asilimia 100 kwa nini isiwezekane?

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
3m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
32m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’