BMT yaridhia rasimu ya Katiba Simba

Joel JJ By Joel JJ β€’ 18th January 2024


BMT yaridhia rasimu ya Katiba Simba

Baada ya mvutano wa miaka kadhaa hatimaye Baraza la Michezo la Taifa (BMT) limeridhia rasimu ya Katiba ya klabu ya Simba ikiwa ni hatua muhimu kuelekea kukamilika kwa mchakato wa Mabadiliko uliochukua takribani miaka mitano

Akizungumza katika Mkutano na Wanahabari mapema leo, Mwenyekiti wa kamati ya Katiba na Sheria wa Simba, Hussein Kitta amesema kamati yake imepokea barua kutoka BMT ikieleza kuridhishwa na yale yaliyopitishwa katika rasimu ya Katiba baada ya kufanyiwa marekebisho

Kitta amesema hayo yamefikiwa baada ya jitihada za pamoja kati ya Wizara yenye dhamana ya Michezo na Klabu ya Simba

"Waziri mwenye dhamana ya michezo aliitisha kikao kujadili kuhusu mchakato wa mabadiliko wa Simba na kukawa na mambo sita ambayo yanatakiwa kufanyiwa kazi"

"Kutokana na mkutano huo, bodi ya Simba ikaunda kamati hii. Tulipokea maoni mengi, mengine kwa barua pepe, mengine kwa barua, wengine kutupigia simu na kutumia ujumbe. Tulikaa vikao vinne kwa kati ya masaa 4-9"

"Lengo ni kukamilisha mabadiliko na serikali ilitupa muda ili kukamilisha jambo hili. BMT walisema kabla ya kupeleka kwa wanachama mlete hiyo rasimu tupitie kwanza. Baada ya vikao tukaenda BMT na nina furaha kuwambia kwamba tumepokea barua kutoka kwao ya kuridhishwa na yale tuliyopitisha"

"Mambo sita yaliyopitishwa yana faida zaidi kwa mwanachama wa Simba kuliko kwa mtu mwingine yoyote," alisema Kitta


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.