Ni ushindi tu dhidi ya DR Congo leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 24th January 2024


Ni ushindi tu dhidi ya DR Congo leo

Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' leo inaweza kuandka rekodi mpya ya kufuzu hatua ya mtoano michuano ya Afcon 2023 inayoendelea huko Ivory Coast katika mchezo dhidi ya DR Congo

Tanzania inahitaji kushinda mchezo huo ili kujihakikishia tiketi hiyo na itakuwa ni mara ya kwanza kufikia mafanikio hayo

Hii ni mara ya tatu Tanzania inashiriki Afcon na tayari imefanikiwa kupata alama moja jambo ambalo halikuwezekana katika awamu mbili zilizopita

Kaimu Kocha Mkuu wa Tanzania Hamed Morocco amesema wanakwenda katika mchezo huo wakiwa na lengo moja la kusaka ushindi huku nahodha wa kikosi hicho Mbwana Samatta akiahidi timu kupambana ili kuhakikisha wanapata matokeo muhimu ambayo yatawavusha

Mechi haitarajiwi kuwa nyepesi kwani DR Congo wenye alama mbili pia wanahitaji ushindi ili kusonga mbele

Alama moja pia inaweza kuwatosha DR Congo kusonga mbele kupitia 'best looser' kama itatokea Zambia kuifunga Morocco katika mchezo mwingine

Kila la kheri Taifa Stars, kila la kheri Tanzania


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.