Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' leo inaweza kuandka rekodi mpya ya kufuzu hatua ya mtoano michuano ya Afcon 2023 inayoendelea huko Ivory Coast katika mchezo dhidi ya DR Congo
Tanzania inahitaji kushinda mchezo huo ili kujihakikishia tiketi hiyo na itakuwa ni mara ya kwanza kufikia mafanikio hayo
Hii ni mara ya tatu Tanzania inashiriki Afcon na tayari imefanikiwa kupata alama moja jambo ambalo halikuwezekana katika awamu mbili zilizopita
Kaimu Kocha Mkuu wa Tanzania Hamed Morocco amesema wanakwenda katika mchezo huo wakiwa na lengo moja la kusaka ushindi huku nahodha wa kikosi hicho Mbwana Samatta akiahidi timu kupambana ili kuhakikisha wanapata matokeo muhimu ambayo yatawavusha
Mechi haitarajiwi kuwa nyepesi kwani DR Congo wenye alama mbili pia wanahitaji ushindi ili kusonga mbele
Alama moja pia inaweza kuwatosha DR Congo kusonga mbele kupitia 'best looser' kama itatokea Zambia kuifunga Morocco katika mchezo mwingine
Kila la kheri Taifa Stars, kila la kheri Tanzania



