TPLB kutangaza tarehe ya Ligi kurejea

Joel JJ By Joel JJ β€’ 26th January 2024


TPLB kutangaza tarehe ya Ligi kurejea

Bodi ya Ligi wakati wowote itatangaza kuendelea kwa ratiba baada ya timu za Taifa za Tanzania na Zambia kutolewa katika michuano ya Afcon 2023 inayoendelea huko Ivory Coast

Mtendaji Mkuu wa Bodi Almas Kasongo amesema wakati wowote kuanzia leo watatangaza tarehe ya ligi hiyo kurejea

Kasongo amesema kwa mujibu wa kanuni timu ambayo itakuwa na kuanzia wachezaji watatu katika timu ya Taifa, mechi zake zitasimama lakini kwa sasa hakuna timu ya ligi kuu ambayo ina wachezaji watatu au zaidi katika timu za Taifa

"Kama tulivosema toka awali, Ligi yetu itarejea rasmi pale tutakapokuwa tumerejea kutoka kwenye fainali za Afcon 2023, muhimu tunazingatia kanuni"

"Endapo klabu itakuwa na wachezaji wasiopungua watatu kwenye timu ya taifa maana yake michezo yake itasimama lakini kwa mazingira ambayo tunayo hulioni tena hilo"

"Kesho (leo) tutakaa kama Bodi kufanya majumuisho na kutangaza rasmi tarehe ya kurudi kwa Ligi Kuu ya NBC. Tunarudi vipi? tutarudi pale tulpoishia," alisema Kasongo


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.