Yanga mikononi mwa Dodoma Jiji leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th February 2024


Yanga mikononi mwa Dodoma Jiji leo

Baada ya kupoteza alama mbili mkoani Kagera, leo Yanga ina mtihani mwingine mbele ya Dodoma Jiji katika mchezo wa ligi kuu ya NBC ambao utapigwa uwanja wa Azam Complex

Ni mtihani kwa sababu Dodoma Jiji hajawahi kuwa mpinzani mwepesi kwa Yanga licha ya Wananchi kuwa na matokeo mazuri dhidi yao

Mara ya mwisho timu hizo kukutana dimba la Azam Complex ni msimu uliopita ambapo Yanga ililazimika kutokea nyuma na kuibuka na ushindi wa jiooooni wa mabao 4-2 ambao uliwahakikishia Wananchi ubingwa wa 29 Ligi Kuu ya NBC

Wakati huu Dodoma Jiji wanakuja kuchuana na Yanga wakiwa na kocha mpya, Francis Baraza aliyewahi kuzinoa Kagera Sugar na Biashara United kabla ya kurejea kwao Kenya

Mkufunzi wa Yanga Miguel Gamondi anafahamu leo wanazihitaji alama zote tatu ili kurejea kileleni mwa msimamo wa ligi

Matokeo tofauti na ushindi yanaweza kupelekea presha kubwa kutoka kwa mashabiki wa timu hiyo ambao hawakufurahishwa na kiwango kilichoonyeshwa na timu yao katika mchezo uliopita

Mchezo huo utapigwa kuanzia saa 1 usiku


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.