Ivory Coast - Local - Nigeria - International

Haller aipa Ivory Coast ubingwa Afcon 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
12 Feb 2024
Haller aipa Ivory Coast ubingwa Afcon 2023

Usiku wa kuamkia leo, Sebastien Haller alikuwa shujaa wa Ivory Coast  wakati The Elephants walipotoka nyuma na kuwashinda Nigeria mabao 2-1 na kushinda fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika 2023 wakiwa nyumbani

Mshambulizi huyo, ambaye pia alifunga bao la ushindi wa nusu fainali, aliunganisha krosi ya Simon Adingra zikiwa zimesalia dakika tisa kukamilisha mchezo huo kipindi cha pili na kuibua shangwe kali jijini Abidjan

William Troost-Ekong alikuwa ameiweka Nigeria mbele dakika saba kabla ya kumalizika kwa kipindi cha kwanza wakati beki huyo wa kati aliporuka juu zaidi na kufunga kwa kichwa

Franck Kessie alifunga bao la kusawazisha dakika ya 62 kutokana na kona ya Adingra ambaye alitajwa kuwa mchezaji bora chipukizi wa michuano hiyo

Ivory Coast haikuwa na mwanzo mzuri katika michuano hiyo ikipenya hatua ya 16 kupitia 'best looser' lakini baadae kila kitu kikabadilika hadi kuwa mabingwa

Ivory Coast walinyakua taji la tatu la bara na ushindi waliosatahili kuupata

More Stories

Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
28m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
22h ago
READ MORE β†’