Simba yajipanga kusaka ushindi Ivory Coast

Joel JJ By Joel JJ β€’ 17th February 2024


Simba yajipanga kusaka ushindi Ivory Coast

Baada ya mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar kusogezwa mbele, Simba sasa inaelekeza nguvu zake katika mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Asec Mimosas ambao utapigwa Ijumaa, Februari 23 huko Ivory Coast

Huu ni mchezo muhimu sana kwa Simba ambayo inapiga hesabu za kutinga robo fainali ya michuano hiyo

Simba ikiwa na alama tano katika nafasi ya pili, inahitaji ushindi au hata alama moja tu ili kuwa katika nafasi nzuri ya kufuzu robo fainali

Ni mechi ambayo Simba haipaswi kupoteza kwa gharama yoyote kwani matokeo hayo yatarejesha matumaini ya Wydad kusonga mbele

Wydad wana alama tatu ambapo kama watashinda mechi mbili zilizobaki watafikisha alama tisa

Simba itaweza kufikisha alama tisa kama itapata sare Ivory Coast na kushinda mechi ya mwisho nyumbani dhidi ya Jwaneng Galaxy na inaweza kufikisha alama 11 kama itashinda mechi zote mbili zilizobaki


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.