Yanga mikononi mwa KMC, NBC PL

Joel JJ By Joel JJ β€’ 17th February 2024


Yanga mikononi mwa KMC, NBC PL

Mabingwa wa soka Tanzania Bara Yanga leo wako mkoani Morogoro kumenyana na KMC katika mchezo wa ligi kuu ya NBC

Baada ya kukamilika mechi 15 za duru ya kwanza, Yanga inaanza kampeni ya kusaka alama 45 za nusu ya pili ya msimu

Wananchi wataingia kwenye mchezo huo wakiwa na kumbukumbu ya ushindi wa mabao 5-0 waliopata katika mchezo wa duru ya kwanza lakini ni wazi mechi ya leo itakuwa tofauti

KMC ni mongoni mwa timu zinazofanya vizuri msimu huu ikiwa imepoteza mechi tatu tu. Adhabu waliyopata katika mchezo wa kwanza itawafanya waingie tofauti leo

Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amesema anatambua mchezo huo hautakuwa rahisi lakini wamejipanga kuwapa furaha mashabiki wao na kuibuka na ushindi

Mchezo utapigwa saa 10 jioni..


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.