Mabingwa wa soka Tanzania Bara Yanga leo wako mkoani Morogoro kumenyana na KMC katika mchezo wa ligi kuu ya NBC
Baada ya kukamilika mechi 15 za duru ya kwanza, Yanga inaanza kampeni ya kusaka alama 45 za nusu ya pili ya msimu
Wananchi wataingia kwenye mchezo huo wakiwa na kumbukumbu ya ushindi wa mabao 5-0 waliopata katika mchezo wa duru ya kwanza lakini ni wazi mechi ya leo itakuwa tofauti
KMC ni mongoni mwa timu zinazofanya vizuri msimu huu ikiwa imepoteza mechi tatu tu. Adhabu waliyopata katika mchezo wa kwanza itawafanya waingie tofauti leo
Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amesema anatambua mchezo huo hautakuwa rahisi lakini wamejipanga kuwapa furaha mashabiki wao na kuibuka na ushindi
Mchezo utapigwa saa 10 jioni..



