Msafara uliojumuisha wachezaji 22 wa Simba, uliondoka Tanzania Alfajiri ya leo Jumanne kuelekea Ivory Coast kwa ajili ya mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Asec Mimosas
Kocha Mkuu wa Simba Abdelhak Benchikha alibainisha kuwa wanakwenda Ivory Coast kukabiliana na moja ya timu bora barani Afrika kwa sasa lakini watapambana kuhakikisha wanapata matokeo mazuri
Simba inawania nafasi ya kutinga robo fainali ambapo ili kuweka hai matumaini yake, lazima wahakikishe hawapotezi mchezo huko Ivory Coast
Simba iko nafasi ya pili kundi B ikiwa na alama tano nyuma ya Asec yenye alama 10 ikiwa tayari imetinga robo fainali
Jwaneng Galaxy inashika nafasi ya tatu ikiwa na alama nne wakati Wydad wanaburuza mkia wakiwa na alama tatu



