Simba yapaa Ivory Coast na matumaini ya ushindi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 20th February 2024


Simba yapaa Ivory Coast na matumaini ya ushindi

Msafara uliojumuisha wachezaji 22 wa Simba, uliondoka Tanzania Alfajiri ya leo Jumanne kuelekea Ivory Coast kwa ajili ya mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Asec Mimosas

Kocha Mkuu wa Simba Abdelhak Benchikha alibainisha kuwa wanakwenda Ivory Coast kukabiliana na moja ya timu bora barani Afrika kwa sasa lakini watapambana kuhakikisha wanapata matokeo mazuri

Simba inawania nafasi ya kutinga robo fainali ambapo ili kuweka hai matumaini yake, lazima wahakikishe hawapotezi mchezo huko Ivory Coast

Simba iko nafasi ya pili kundi B ikiwa na alama tano nyuma ya Asec yenye alama 10 ikiwa tayari imetinga robo fainali

Jwaneng Galaxy inashika nafasi ya tatu ikiwa na alama nne wakati Wydad wanaburuza mkia wakiwa na alama tatu


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.