Klabu ya Azam Fc iko katika maombolezo kufuatia kifo cha aliyekuwa Daktari wa timu hiyo Dk Mwanandi Mwankemwa kilichotokea hapo jana
Kifo cha Dk Mwankemwa ni pigo kubwa kwa mpira wa miguu nchini kwani amekuwa Mwanafamilia kwa zaidi ya miaka 15
Kulingana na taarifa iliyotolewa na Azam Fc, maziko ya Dk Mwankemwa, yatafanyika kesho Alhamisi Februari 29, saa 7 mchana kwenye makaburi ya Kinondoni
Mwili wa marehemu utatokea nyumbani kwake Mwanagati, Temeke, Dar es Salaam
Inna Lillah Wainna Ilayhi Rajiun!



