Pumzika kwa Amani Dk Mwankemwa

Joel JJ By Joel JJ β€’ 28th February 2024


Pumzika kwa Amani Dk Mwankemwa

Klabu ya Azam Fc iko katika maombolezo kufuatia kifo cha aliyekuwa Daktari wa timu hiyo Dk Mwanandi Mwankemwa kilichotokea hapo jana

Kifo cha Dk Mwankemwa ni pigo kubwa kwa mpira wa miguu nchini kwani amekuwa Mwanafamilia kwa zaidi ya miaka 15

Kulingana na taarifa iliyotolewa na Azam Fc, maziko ya Dk Mwankemwa, yatafanyika kesho Alhamisi Februari 29, saa 7 mchana kwenye makaburi ya Kinondoni

Mwili wa marehemu utatokea nyumbani kwake Mwanagati, Temeke, Dar es Salaam

Inna Lillah Wainna Ilayhi Rajiun!


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.